بِسْمِ اللَّهِ الرَّحْمَٰنِ الرَّحِيمِ
Bismillahir Rahmanir Rahim
Kwa jina la Mwenyezi Mungu Mwingi wa Rehema Mwenye Kurehemu
الحَمْـدُ لِلّهِ الّذي أَحْـيانا بَعْـدَ ما أَماتَـنا وَإليه النُّـشور
AlhamduliLLaahil-LLadhiy Ahyaanaa ba’da maa amaatana wa Ilayhin-nushuwr
Himdi Anastahiki Allaah Ambaye Ametupa uhai baada ya kutufisha na ni Kwake tu kufufuliwa.
الحمدُ للهِ الّذي كَساني هذا (الثّوب) وَرَزَقَنيه مِنْ غَـيـْرِ حَولٍ مِنّي وَلا قـوّة
AlhamduliLLaahil lladhiyy kasaaniy haadha (ath-thawb) warazaqaniyhi min ghayri hawlin minniy walaa quwwah
Himdi Anastahiki Allaah Ambaye Amenivisha nguo hii, na kuniruzuku pasina uwezo kutoka kwangu wala nguvu
بِسْمِ الله
BismiLLaah
Kwa jina la Allaah
(بِسْمِ الله) اللّهُـمَّ إِنِّـي أَعـوذُ بِـكَ مِـنَ الْخُـبْثِ وَالْخَبائِث
(BismilLLaah) Allaahumma inniy a’uwdhu Bika minal khubthi wal khabaaith
(Kwa jina la Allaah) Ee Allaah najikinga kwako kutokana na mashaytwaan ya kiume na ya kike
غُفْـرانَك
Ghufraanak
Nakuomba maghfira