Al-Qari'ah
القارعة
11 AyaMakki

بِسْمِ ٱللَّهِ ٱلرَّحْمَٰنِ ٱلرَّحِيمِ

Kwa jina la Mwenyezi Mungu, Mwingi wa rehema, Mwenye kurehemu

1

ٱلْقَارِعَةُ

Inayo gonga!

2

مَا ٱلْقَارِعَةُ

Nini Inayo gonga?

3

وَمَآ أَدْرَىٰكَ مَا ٱلْقَارِعَةُ

Na nini kitacho kujuilisha nini Inayo gonga?

4

يَوْمَ يَكُونُ ٱلنَّاسُ كَٱلْفَرَاشِ ٱلْمَبْثُوثِ

Siku ambayo watu watakuwa kama nondo walio tawanyika;

5

وَتَكُونُ ٱلْجِبَالُ كَٱلْعِهْنِ ٱلْمَنفُوشِ

Na milima itakuwa kama sufi zilizo chambuliwa!

6

فَأَمَّا مَن ثَقُلَتْ مَوَٰزِينُهُۥ

Basi yule ambaye mizani yake itakuwa nzito,

7

فَهُوَ فِى عِيشَةٍۢ رَّاضِيَةٍۢ

Huyo atakuwa katika maisha ya kupendeza.

8

وَأَمَّا مَنْ خَفَّتْ مَوَٰزِينُهُۥ

Na yule ambaye mizani yake itakuwa khafifu,

9

فَأُمُّهُۥ هَاوِيَةٌۭ

Huyo maskani yake yatakuwa Moto wa Hawiya!

10

وَمَآ أَدْرَىٰكَ مَا هِيَهْ

Na nini kitacho kujuilisha nini hiyo?

11

نَارٌ حَامِيَةٌۢ

Ni Moto mkali!