At-Takathur
التكاثر
8 AyaMakki
بِسْمِ ٱللَّهِ ٱلرَّحْمَٰنِ ٱلرَّحِيمِ
Kwa jina la Mwenyezi Mungu, Mwingi wa rehema, Mwenye kurehemu
1
أَلْهَىٰكُمُ ٱلتَّكَاثُرُ
Kumekushughulisheni kutafuta wingi,
2
حَتَّىٰ زُرْتُمُ ٱلْمَقَابِرَ
Mpaka mje makaburini!
3
كَلَّا سَوْفَ تَعْلَمُونَ
Sivyo hivyo! Mtakuja jua!
4
ثُمَّ كَلَّا سَوْفَ تَعْلَمُونَ
Tena sivyo hivyo! Mtakuja jua!
5
كَلَّا لَوْ تَعْلَمُونَ عِلْمَ ٱلْيَقِينِ
Sivyo hivyo! Lau mngeli jua kwa ujuzi wa yakini,
6
لَتَرَوُنَّ ٱلْجَحِيمَ
Basi bila ya shaka mtaiona Jahannamu!
7
ثُمَّ لَتَرَوُنَّهَا عَيْنَ ٱلْيَقِينِ
Tena, bila ya shaka, mtaiona kwa jicho la yakini.
8
ثُمَّ لَتُسْـَٔلُنَّ يَوْمَئِذٍ عَنِ ٱلنَّعِيمِ
Tena bila ya shaka mtaulizwa siku hiyo juu ya neema.