Al-'Asr
العصر
3 AyaMakki
بِسْمِ ٱللَّهِ ٱلرَّحْمَٰنِ ٱلرَّحِيمِ
Kwa jina la Mwenyezi Mungu, Mwingi wa rehema, Mwenye kurehemu
1
وَٱلْعَصْرِ
Naapa kwa Zama!
2
إِنَّ ٱلْإِنسَٰنَ لَفِى خُسْرٍ
Hakika binaadamu bila ya shaka yumo katika khasara,
3
إِلَّا ٱلَّذِينَ ءَامَنُوا۟ وَعَمِلُوا۟ ٱلصَّٰلِحَٰتِ وَتَوَاصَوْا۟ بِٱلْحَقِّ وَتَوَاصَوْا۟ بِٱلصَّبْرِ
Ila wale walio amini, na wakatenda mema, na wakausiana kwa haki, na wakausiana kusubiri.