Al-Humazah
الهمزة
9 AyaMakki

بِسْمِ ٱللَّهِ ٱلرَّحْمَٰنِ ٱلرَّحِيمِ

Kwa jina la Mwenyezi Mungu, Mwingi wa rehema, Mwenye kurehemu

1

وَيْلٌۭ لِّكُلِّ هُمَزَةٍۢ لُّمَزَةٍ

Ole wake kila safihi, msengenyaji!

2

ٱلَّذِى جَمَعَ مَالًۭا وَعَدَّدَهُۥ

Aliye kusanya mali na kuyahisabu.

3

يَحْسَبُ أَنَّ مَالَهُۥٓ أَخْلَدَهُۥ

Anadhani ya kuwa mali yake yatambakisha milele!

4

كَلَّا ۖ لَيُنۢبَذَنَّ فِى ٱلْحُطَمَةِ

Hasha! Atavurumishwa katika H'ut'ama.

5

وَمَآ أَدْرَىٰكَ مَا ٱلْحُطَمَةُ

Na nani atakujuvya ni nini H'ut'ama?

6

نَارُ ٱللَّهِ ٱلْمُوقَدَةُ

Moto wa Allah ulio washwa.

7

ٱلَّتِى تَطَّلِعُ عَلَى ٱلْأَفْـِٔدَةِ

Ambao unapanda nyoyoni.

8

إِنَّهَا عَلَيْهِم مُّؤْصَدَةٌۭ

Hakika huo utafungiwa nao

9

فِى عَمَدٍۢ مُّمَدَّدَةٍۭ

Kwenye nguzo zilio nyooshwa.