Al-Ma'un
الماعون
7 AyaMakki
بِسْمِ ٱللَّهِ ٱلرَّحْمَٰنِ ٱلرَّحِيمِ
Kwa jina la Mwenyezi Mungu, Mwingi wa rehema, Mwenye kurehemu
1
أَرَءَيْتَ ٱلَّذِى يُكَذِّبُ بِٱلدِّينِ
Je! Umemwona anaye kadhibisha Malipo?
2
فَذَٰلِكَ ٱلَّذِى يَدُعُّ ٱلْيَتِيمَ
Huyo ndiye anaye msukuma yatima,
3
وَلَا يَحُضُّ عَلَىٰ طَعَامِ ٱلْمِسْكِينِ
Wala hahimizi kumlisha masikini.
4
فَوَيْلٌۭ لِّلْمُصَلِّينَ
Basi, ole wao wanao sali,
5
ٱلَّذِينَ هُمْ عَن صَلَاتِهِمْ سَاهُونَ
Ambao wanapuuza Sala zao;
6
ٱلَّذِينَ هُمْ يُرَآءُونَ
Ambao wanajionyesha,
7
وَيَمْنَعُونَ ٱلْمَاعُونَ
Nao huku wanazuia msaada.