Al-Ma'un
الماعون
7 AyaMakki

بِسْمِ ٱللَّهِ ٱلرَّحْمَٰنِ ٱلرَّحِيمِ

Kwa jina la Mwenyezi Mungu, Mwingi wa rehema, Mwenye kurehemu

1

أَرَءَيْتَ ٱلَّذِى يُكَذِّبُ بِٱلدِّينِ

Je! Umemwona anaye kadhibisha Malipo?

2

فَذَٰلِكَ ٱلَّذِى يَدُعُّ ٱلْيَتِيمَ

Huyo ndiye anaye msukuma yatima,

3

وَلَا يَحُضُّ عَلَىٰ طَعَامِ ٱلْمِسْكِينِ

Wala hahimizi kumlisha masikini.

4

فَوَيْلٌۭ لِّلْمُصَلِّينَ

Basi, ole wao wanao sali,

5

ٱلَّذِينَ هُمْ عَن صَلَاتِهِمْ سَاهُونَ

Ambao wanapuuza Sala zao;

6

ٱلَّذِينَ هُمْ يُرَآءُونَ

Ambao wanajionyesha,

7

وَيَمْنَعُونَ ٱلْمَاعُونَ

Nao huku wanazuia msaada.