Al-Masad
المسد
5 AyaMakki
بِسْمِ ٱللَّهِ ٱلرَّحْمَٰنِ ٱلرَّحِيمِ
Kwa jina la Mwenyezi Mungu, Mwingi wa rehema, Mwenye kurehemu
1
تَبَّتْ يَدَآ أَبِى لَهَبٍۢ وَتَبَّ
Imeangamia mikono ya Abu Lahab, na yeye pia ameangamia.
2
مَآ أَغْنَىٰ عَنْهُ مَالُهُۥ وَمَا كَسَبَ
Hayatamfaa mali yake, wala alivyo vichuma.
3
سَيَصْلَىٰ نَارًۭا ذَاتَ لَهَبٍۢ
Atauingia Moto wenye mwako.
4
وَٱمْرَأَتُهُۥ حَمَّالَةَ ٱلْحَطَبِ
Na mkewe, mchukuzi wa kuni,
5
فِى جِيدِهَا حَبْلٌۭ مِّن مَّسَدٍۭ
Shingoni mwake iko kamba iliyo sokotwa.