Al-Falaq
الفلق
5 AyaMakki

بِسْمِ ٱللَّهِ ٱلرَّحْمَٰنِ ٱلرَّحِيمِ

Kwa jina la Mwenyezi Mungu, Mwingi wa rehema, Mwenye kurehemu

1

قُلْ أَعُوذُ بِرَبِّ ٱلْفَلَقِ

Sema: Najikinga kwa Mola Mlezi wa mapambazuko,

2

مِن شَرِّ مَا خَلَقَ

Na shari ya alivyo viumba,

3

وَمِن شَرِّ غَاسِقٍ إِذَا وَقَبَ

Na shari ya giza la usiku liingiapo,

4

وَمِن شَرِّ ٱلنَّفَّٰثَٰتِ فِى ٱلْعُقَدِ

Na shari ya wanao pulizia mafundoni,

5

وَمِن شَرِّ حَاسِدٍ إِذَا حَسَدَ

Na shari ya hasidi anapo husudu.