Ad-Duha
الضحى
11 AyaMakki

بِسْمِ ٱللَّهِ ٱلرَّحْمَٰنِ ٱلرَّحِيمِ

Kwa jina la Mwenyezi Mungu, Mwingi wa rehema, Mwenye kurehemu

1

وَٱلضُّحَىٰ

Naapa kwa mchana!

2

وَٱلَّيْلِ إِذَا سَجَىٰ

Na kwa usiku unapo tanda!

3

مَا وَدَّعَكَ رَبُّكَ وَمَا قَلَىٰ

Mola wako Mlezi hakukuacha, wala hakukasirika nawe.

4

وَلَلْءَاخِرَةُ خَيْرٌۭ لَّكَ مِنَ ٱلْأُولَىٰ

Na bila ya shaka wakati ujao utakuwa bora kwako kuliko ulio tangulia.

5

وَلَسَوْفَ يُعْطِيكَ رَبُّكَ فَتَرْضَىٰٓ

Na Mola wako Mlezi atakupa mpaka uridhike.

6

أَلَمْ يَجِدْكَ يَتِيمًۭا فَـَٔاوَىٰ

Kwani hakukukuta yatima akakupa makaazi?

7

وَوَجَدَكَ ضَآلًّۭا فَهَدَىٰ

Na akakukuta umepotea akakuongoa?

8

وَوَجَدَكَ عَآئِلًۭا فَأَغْنَىٰ

Akakukuta mhitaji akakutosheleza?

9

فَأَمَّا ٱلْيَتِيمَ فَلَا تَقْهَرْ

Basi yatima usimwonee!

10

وَأَمَّا ٱلسَّآئِلَ فَلَا تَنْهَرْ

Na anaye omba au kuuliza usimkaripie!

11

وَأَمَّا بِنِعْمَةِ رَبِّكَ فَحَدِّثْ

Na neema za Mola wako Mlezi zisimlie.