Ash-Sharh
الشرح
8 AyaMakki
بِسْمِ ٱللَّهِ ٱلرَّحْمَٰنِ ٱلرَّحِيمِ
Kwa jina la Mwenyezi Mungu, Mwingi wa rehema, Mwenye kurehemu
1
أَلَمْ نَشْرَحْ لَكَ صَدْرَكَ
Hatukukunjulia kifua chako?
2
وَوَضَعْنَا عَنكَ وِزْرَكَ
Na tukakuondolea mzigo wako,
3
ٱلَّذِىٓ أَنقَضَ ظَهْرَكَ
Ulio vunja mgongo wako?
4
وَرَفَعْنَا لَكَ ذِكْرَكَ
Na tukakunyanyulia utajo wako?
5
فَإِنَّ مَعَ ٱلْعُسْرِ يُسْرًا
Basi kwa hakika pamoja na uzito upo wepesi,
6
إِنَّ مَعَ ٱلْعُسْرِ يُسْرًۭا
Hakika pamoja na uzito upo wepesi.
7
فَإِذَا فَرَغْتَ فَٱنصَبْ
Na ukipata faragha, fanya juhudi.
8
وَإِلَىٰ رَبِّكَ فَٱرْغَب
Na Mola wako Mlezi ndio mshughulikie.