At-Tin
التين
8 AyaMakki

بِسْمِ ٱللَّهِ ٱلرَّحْمَٰنِ ٱلرَّحِيمِ

Kwa jina la Mwenyezi Mungu, Mwingi wa rehema, Mwenye kurehemu

1

بِّسْمِ ٱللَّهِ ٱلرَّحْمَٰنِ ٱلرَّحِيمِ وَٱلتِّينِ وَٱلزَّيْتُونِ

Naapa kwa tini na zaituni!

2

وَطُورِ سِينِينَ

Na kwa Mlima wa Sinai!

3

وَهَٰذَا ٱلْبَلَدِ ٱلْأَمِينِ

Na kwa mji huu wenye amani!

4

لَقَدْ خَلَقْنَا ٱلْإِنسَٰنَ فِىٓ أَحْسَنِ تَقْوِيمٍۢ

Bila ya shaka tumemuumba mtu kwa umbo lilio bora kabisa.

5

ثُمَّ رَدَدْنَٰهُ أَسْفَلَ سَٰفِلِينَ

Kisha tukamrudisha kuwa chini kuliko walio chini!

6

إِلَّا ٱلَّذِينَ ءَامَنُوا۟ وَعَمِلُوا۟ ٱلصَّٰلِحَٰتِ فَلَهُمْ أَجْرٌ غَيْرُ مَمْنُونٍۢ

Lakini wale walio amini na wakatenda mema, hao watapata ujira usio kwisha.

7

فَمَا يُكَذِّبُكَ بَعْدُ بِٱلدِّينِ

Basi ni kipi baadaye kitacho kukukadhibishia malipo?

8

أَلَيْسَ ٱللَّهُ بِأَحْكَمِ ٱلْحَٰكِمِينَ

Kwani Allah si muadilifu kuliko mahakimu wote?