Az-Zalzalah
الزلزلة
8 AyaMadani

بِسْمِ ٱللَّهِ ٱلرَّحْمَٰنِ ٱلرَّحِيمِ

Kwa jina la Mwenyezi Mungu, Mwingi wa rehema, Mwenye kurehemu

1

إِذَا زُلْزِلَتِ ٱلْأَرْضُ زِلْزَالَهَا

Itakapo tetemeshwa ardhi kwa mtetemeko wake!

2

وَأَخْرَجَتِ ٱلْأَرْضُ أَثْقَالَهَا

Na itakapo toa ardhi mizigo yake!

3

وَقَالَ ٱلْإِنسَٰنُ مَا لَهَا

Na mtu akasema: Ina nini?

4

يَوْمَئِذٍۢ تُحَدِّثُ أَخْبَارَهَا

Siku hiyo itahadithia khabari zake.

5

بِأَنَّ رَبَّكَ أَوْحَىٰ لَهَا

Kwa sababu Mola wake Mlezi ameifunulia!

6

يَوْمَئِذٍۢ يَصْدُرُ ٱلنَّاسُ أَشْتَاتًۭا لِّيُرَوْا۟ أَعْمَٰلَهُمْ

Siku hiyo watu watatoka kwa mfarakano wakaonyweshwe vitendo vyao!

7

فَمَن يَعْمَلْ مِثْقَالَ ذَرَّةٍ خَيْرًۭا يَرَهُۥ

Basi anaye tenda chembe ya wema, atauona!

8

وَمَن يَعْمَلْ مِثْقَالَ ذَرَّةٍۢ شَرًّۭا يَرَهُۥ

Na anaye tenda chembe ya uovu atauona!